Watu waliokimbia makazi yao wanaoishi katika kambi ya Plaine Savo, karibu na Fataki, katika eneo la Djugu, bado wako katika hatari kubwa ya ukatili na mashambulizi.
Katika taarifa iliyotolewa tarehe 8 Septemba 2026, Médecins Sans Frontières (MSF) inasema kuwa, katika miezi sita iliyopita, kituo cha afya kinachosaidiwa na MSF kilipokea karibu waathirika 60 wa ukatili wa kingono kila mwezi, pamoja na watu 7 walioumia kwa risasi au silaha za kukatia kila wiki.
Kwa mujibu wa MSF, baadhi ya waathirika walishambuliwa wakati walipotoka kambini kwenda mashambani, kutafuta kuni au kutafuta mahitaji ya familia zao.
Hali hii ya ukosefu wa usalama pia inafanya watu washindwe kufikia mashamba yao na kuongeza tatizo la chakula. MSF inasema kuwa karibu watu 9 wapya wenye ugonzwa sababu ya ukosefu wa chakula wanapokelewa kila wiki katika eneo hilo.
MSF inatoa wito wa kuimarisha ulinzi wa wakimbizi wa ndani na kuruhusu mashirika ya kibinadamu kufikia zaidi watu walio katika mazingira magumu.
Muandishi
![]()
- Partager sur Facebook(ouvre dans une nouvelle fenêtre) Facebook
- Partager sur X(ouvre dans une nouvelle fenêtre) X
- Envoyer un lien par e-mail à un ami(ouvre dans une nouvelle fenêtre) E-mail
- Partager sur LinkedIn(ouvre dans une nouvelle fenêtre) LinkedIn
- Partager sur X(ouvre dans une nouvelle fenêtre) X
- Partager sur Pinterest(ouvre dans une nouvelle fenêtre) Pinterest
- Partager sur Telegram(ouvre dans une nouvelle fenêtre) Telegram
- Partager sur WhatsApp(ouvre dans une nouvelle fenêtre) WhatsApp



















